Aliyekuwa mgombea wa kiti cha Ubunge wa Kinondoni kwa tiketi ya chama cha ACT Wazalendo, Kalama Masoud aka Kala Pina amefungua kesi mahakamani ya kupinga matokeo hayo.
“Kiukweli matokeo yale ya Jimbo la Kinondoni sikubaliano nayo kutokana na mapungufu ambayo yalikuwa yamejitokeza katika uchaguzi… kulikuwa na mapungufu mengi ikiwemo kutishwa kwa mawakala wangu katika kata ya Tandale kilichopelekea baadhi ya mawakala wangu kuondoka na wengi walikuwa akina mama” ameimbia Millard ayo
“Nimeazimia kuupinga uchaguzi huu kwa kwenda Mahakamani kwa sababu naona Demokrasia haikutumika ipasavyo na iliminywa… kuna baadhi ya maeneo watu wanalalamika wamekimbilia Mahakamani kutokana na matokeo yasiyo sahihi, na mimi mwenyewe natarajia kwenda kusikiliza hii kesi Mahakamani wiki ijayo” Aliongeza Kla pina
Source: Millardayo.com